• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Halmashauri ya Wilaya ya Geita
Halmashauri ya Wilaya ya Geita

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya msingi
    • Mikakati
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo
    • Idara
      • Utawala
      • Mipango Takwimu na Ufuatiliaji
        • TASAF
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Maji
      • Kilimo Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Maendeleo ya Jamii
      • Afya
      • Elimu Msingi
        • Utamaduni
      • Elimu Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Ardhi na Maliasili
    • Vitengo
      • TEHAMA
      • Manunuzi na Ugavi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • UKIMWI
  • Fursa za uwekezaji
    • Vivutio vya kitalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
    • Viwanda
    • Biashara
  • Huduma zetu
    • Afya
    • Elimu
    • Uvuvi
    • Maji
    • Kilimo
    • Mifugo
    • Ujenzi
  • Madiwani
    • Orodha ya Wahe.Madiwani
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha,Uongozi na Mipango
      • Uchumi,Ujenzi na Mazingira
      • Elimu,Afya na Maji
      • UKIMWI
      • Kamati ya Maadili
    • Ratiba
      • Vikao vya Wahe.Madiwani
      • Kuonana na Mwenyekiti
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi itakayotekelezwa
  • Machapisho
    • Miongozo mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Ripoti mbalimbali
    • Sheria ndogo
    • Mpango mkakati
    • Mkataba wa Huduma kwa Mteja
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa umma
    • Video za shughuli za ofisi/kitaifa
    • Hotuba za viongozi
    • Maktaba ya Picha

UKIMWI

UTEKELEZAJI  WA MPANGO WA Taifa wa KUDHIBITI UKIMWI WILAYA YA GEITA


Mratibu wa Muitikio wa Mapambano dhidi ya UKIMWI Halmashauri ya Wilaya ya Geita

Patricea L.Nsinde


1.0  UTANGULIZI

Halmashauri ya wilaya Geita  inaendelea kutekeleza  kikamilifu shughuli za kupambana  na UKIMWI,ikilenga  kufikia sifuri 3 katika mapambano  dhidi ya UKIMWI ambayo ni kuzuia  maambukizi mapya,kuondoa Unyanyapaa na ubaguzi na kutokomeza vifo vitokanavyo na UKIMWI ifikapo June 2018. Shughuli mbalimbali  ziliandaliwa

kwa kuzingatia maeneo  makuu 3 ya mkakati wa III wa Taifa wa kudhibiti UKIMWI wa mwaka 2013/2014 hadi 2017/2018 ambayo yanalenga :-

•Huduma za kinga

•Mazingira wezeshi

•Kupunguza makali yatokanayo na UKIMWI

2.0 UKIMWI UNAVYOAMBUKIZWA

Kutokana na matokeo ya utafiti uliyofanywa na ofisi ya takwimu ya taifa  mwaka 2012 inaonesha kwamba katika  wilaya yetu Virusi vya UKIMWI vinaambukizwa kwa njia zifuatazo:-

•Kufanya ngono  na mtu mwenye VVU bila kutumia kondomu.

•Kuchangia damu yenye virusi vya UKIMWI.

•Mama mjamzito kumwambukiza mtoto wake aliyetumboni ,wakati wa kujifungua au wakati wa kunyonyesha.


2:1 Maeneo hatarishi yanayochangia kuenea kwa virusi vya UKIMWI:

 Katika wilaya yetu maeneo yenye msongamano wa watu kwa ajili ya shughuli mbalimbali za kiuchumi na kijamii yanaonesha kuwa na kiwango kikubwa cha maambukizi ikilinganishwa na sehemu nyingine.  

Maeneo hayo ni pamoja na:-

•Maeneo ya machimbo ya dhahabu.

•Maeneo ya uvuvi wa samaki kandokando ya ziwa Victoria.

•Vituo vya magari makubwa yanayopita wilayani Geita kwenda mikoa na nchi jirani zinazopakana na nchi yetu.

•Mikusanyiko mbalimbali ya watu hasa nyakati za usiku.

•Maeneo ya kazi  za kiofisi.


2.2 Mila, desturi,tabia na mazingira yanayochochea maambukizi

Baadhi ya mila, desturi na mazingira ya jamii yanachochea maambukizi ambayo ni pamoja na:-

•Ulevi

•Kurithi wajane

•Ndoa za wake wengi

•Ndoa zakulazimishwa(wasichana kuolewa wakiwa na umri mdogo)

•Ngoma za mapacha,bukwilima,kutibiwa kwa waganga wa jadi.

•Mfumo dume

•Asilimia ndogo ya wanaume waliotahiliwa ambao ni asilimia (46%)

•Watumishi walio oana kuishi mbali na wenza wao.

•FEDHA ZILIZOPOKELEWA

•Katika Mwaka wafedha 2015/2016 Halmashauri ya Wilaya iliidhinishiwa bajeti ya Tshs 125,610,000 kuanzia Julai 2015 hadi Aprili 2016 hakuna fedha iliyopokelewa mwaka huo lakini ikapokelewa mwaka wa fedha 2016/2017 ambapo ndipo shughuli zinatekelezwa.Halmashauri iliendelea kukamilisha shughuli chache zilizobaki katika mwaka 2014/2015 ambazo fedha yake ilikuwa jumla ya Tshs 51,600,000/= ambayo ilitumika katika maeneo yafuatayo:-

•

3.0 SHUGHULI ZILIZOTEKELEZWA KATIKA KILA ENEO LA MKAKATI :

•Katika kipindi Julai 2015 hadi Aprili 2016  jumla ya shughuli  13 zimetekelezwa  kwa kila eneo kama ifuatavyo:-

•3.1:ENEO LA HUDUMA ZA KINGA (Tshs 9,734,615 /=)

•i. Kusambaza katoni 164 za kondomu za kiume  katika kata 28.

•ii.  Kuandaa na kuelimisha jamii kwa njia ya sinema katika vijiji 4

•iii. Kuandaa na kufanya majadiliano na wanafunzi324 waelimishajirika wa shule 56 za msingi na 6 za sekondari.

• iv.Kuandaa na kutoa mafunzo kwa wasanii 60 vijana waelimishaji rika nje ya shule.

•3.2 ENEO LA  MAZINGIRA WEZESHI (Tshs 20,867,351 /=)

•i. Kuandaa na kufanya mkutano wa siku 1na viongozi wa jamii 150 juu ya UKIMWI.

•ii.Kufanya ufuatiliaji shirikishi wa shughuli za kudhibiti UKIMWI katika kata 28  wilayani.

•iii.Kuwezesha usimamizi na ukaguzi wa matumizi ya fedha za kudhibiti UKIMWI katika kata 28.

•iv.Kuandaa mpango bajeti na taarifa za utekelezaji za robo 3 na kuwasilisha kwa wakati.

•3.3:ENEO LA  KUPUNGUZA MAKALI YATOKANAYO NA UKIMWI

•Jumla ya Tshs (Tshs 20,000,000/=) zilitumika  kutoa mtaji kwa vikundi 14 vya watu 400 wanaoishi na VVU wenye kipato duni wanaotumia dawa   za ARVs waliyoanzisha miradi  ya uzalishaji mali


5.0  MAFANIKIO:

Katika kipindi hiki mafanikio yaliyopatikana ni :-

•Baadhi ya makundi yaliyo katika mazingira magumu yamepata msaada wa kujikimu.

•Kumekuwa na ongezeko la uelewa kwa jamii kuhusu UKIMWI.

•Mahusiano mazuri kati ya wilaya na wadau mbalimbali ndani na nje ya wilaya.

•Unyanyapaa umepungua katika jamii.

•Jumla ya watoa huduma 31 kwa wagonjwa wa UKIMWI nyumbani wamejengewa uwezo na kukabidhiwa baiskeli 31na shirika la pamoja tuwalee chini ya Jimbo Katoliki Geita.


6.0 CHANGAMOTO

Katika kipindi hiki changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wa shughuli za kupambana na UKIMWI ni pamoja:-

•Kutopata  fedha za utekelezaji wa shughuli zilizopangwa kwa mwaka wa fedha 2015/2016 kutoka Hazina.

• Ongezeko la muingiliano wa watu kutoka sehemu mbalimbali wanaokuja kwa shughuli za kiuchumi kwenye maeneo ya machimbo,visiwani na kandokando ya ziwa.

•Uhaba  wa vitendanishi kwa ajili ya upimaji  walau kwa mama wajawazito.

•Uchache wa wauza kondomu hasa maeneo ya vijijini.

•Ongezeko la vichocheo vya maambukizi kutokana na teknolojia

•Ongezeko la watoto yatima na walio katika mazingira tete.



7.0 MKAKATI NA UTATUZI WA CHANGAMOTO

•Kuongeza jitihada ya kuelimisha jamii kupambana na UKIMWI.

•Kuimarisha  uraghibishi na huduma ya tohara kwa wanaume.

•Kuimarisha ukusanyaji wa rasilimali na kusimamia matumizi bora kwa ajili ya  mapambano dhidi ya UKIMWI

•Kuimarisha  huduma ya ushauri nasaha na upimaji wa virusi vya UKIMWI kwa hiari.

•Kuelimisha na kurahisisha upatikanaji  na usambazaji wa kondom kwa wenye kuzihitaji.

•Kuboresha mfumo wa kutoa  ushauri na misaada kwa walioathirika na kuathiriwa na UKIMWI.

•Kumarisha mfumo wa kukusanya na kusambaza taarifa na takwimu   muhimu zinazohusu UKIMWI.  

•Kuimarisha ushirikiano na wadau na kufanya shughuli zote kwa pamoja.                          

•Kuongeza bajeti ya fedha zitokanazo na vyanzo vya ndani ili kuboresha huduma kwa walengwa.      


MWISHO

Kila mmoja akitimiza wajibu wake Geita bila maambukizi mapya,unyanyapaa na vifo vitokanavyo na UKIMWI Inawezekana.



Tangazo

  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA IMETOA TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI May 24, 2022
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA INAKUTANGAZIA UUZAJI WA VIWANJA ENEO LA MTAKUJA KATIKA MAMLAKA YA MJI MDOGO WA KATORO June 15, 2022
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA IMETOA TANGAZO LA KUWAITA KWENYE USAILI WATENDAJI WA VIJIJI NA MADEREVA June 27, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KAZINI GEITA DC July 08, 2022
  • Tazama zote

Habari Mpya

  • MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI YAWAKUMBUKA AKINA MAMA WALIOJIFUNGUA NA WAFUNGWA WANAWAKE

    March 07, 2023
  • BARAZA LA MADIWANI GEITA DC LAPITISHA BAJETI YA BILIONI 87.2 KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024

    January 24, 2023
  • GEITA DC YAWEKA KAMBI KATIKA KATA YA NYARUGUSU KUTOA MSAADA WA KISHERIA

    December 14, 2022
  • DC SHIMO ATAJA UMOJA NA MSHIKAMANO KUWA NGUZO KUU YA MAENDELEO TUNAPOSHEREHEKEA MIAKA 61 YA UHURU

    December 07, 2022
  • Tazama zote

video

DED. WANGA AWATAKIA MTIHANI MWEMA WANAFUNZI WA KIDATO CHA NNE HALMASHAURI YA WILAYA YA GEITA WANAOJIANDAA KUFANYA MITIHANI YA TAIFA
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Asili ya jina Geita
  • Fursa ya viwanda
  • Fursa ya madini
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA TANO NA VYUO VYA KATI, 2021
  • Vivutio vya Utalii
  • Miradi itakayotekelezwa
  • Miradi inayoendelea
  • Orodha ya wahe.Madiwani

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Ikulu
  • Bofya Hapa Kutuma,Kupokea na Kufuatilia Malalamiko,Mapendekezo,Maulizo na Pongezi Halmashauri ya Wilya ya Geita
  • Tovuti Kuu ya Serikali
  • Watumishi Portal
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu(NBS)
  • Ofisi ya Rais TAMISEMI

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

Counter Widgets

Ramani ya Sehemu

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya ya Geita

    Anuani ya Posta: S.L.P 139 Geita

    Simu: +225 282520061

    Mobile:

    Barua pepe: info@geitadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Privacy Policy
    • Disclamer
    • Maswali na Majibu yanayoulizwa mara kwa mara
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hakimiliki@ Halmashauri ya wilaya ya Geita , Haki zote zimehifadhiwa